Connect with us

Klabu ya soka ya Al Ahly nchini Misri ina nafasi ya kufuzu katika hatua ya mwondoano kuwania taji la klabu bingwa barani Afrika ikiwa itaishinda Wydad Casablanca nchini Morocco siku ya Jumatano.

Itakuwa mara ya kwanza kufika katika hatua hiyo baada ya kufanya hivyo mwaka 2013 na kunyakua taji hilo.

Kocha wa Alhly Hossam El Badry ambaye pia ni mchezaji wa zamani amesema mashabiki wa klabu hiyo wanataka ushindi kwa sababu wanaona wamelikosa taji hilo kwa muda mrefu.

Ahly na Zanaco kutoka Zambia zinaongoza kundi la D kwa alama saba baada ya mechi tatu.

Wydad Casablanca ni wa tatu kwa alama tatu huku Coton Sport ya Cameroon ikiwa haina alama katika kundi hilo.

Ratiba kamili:-
Taji la Shirikisho:

Klabu bingwa

Kundi A:

Kundi B:

Jumanne: Al Merrikh v Ferroviario Beira

Jumatano : Al Ahly Tripoli v CAPS Utd

Jumatano: Al Hilal v Etoile du Sahel

Jumatano: USM Alger v Zamalek

Kundi C:

Kundi D:

Jumanne: AS Vita Club v Saint George

Jumatano : Coton Sport v Zanaco

Jumatano: Esperance v Mamelodi Sundowns

Jumatano: Wydad Casablanca v Al Ahly

More in