Connect with us

AS Vita Club mabingwa ligi kuu ya DRC

AS Vita Club mabingwa ligi kuu ya DRC

Na Victor Abuso,

Klabu ya AS Vita Club nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ndio mabingwa wa ligi kuu ya soka nchini humo msimu huu.

Ligi kuu ya soka nchini humo ilisitishwa kabla ya kuanza kwa mzunguko wa pili na hivyo kuwapa ushindi vijana wa kocha Florent Ibenge.

Mabingwa wa zamani TP Mazembe ni wa pili huku CS Don Bosco ikiwa katika nafasi ya tatu.

Vlabu hivyo vitatu vimefuzu katika michuano ya klabu bingwa na Shirikisho barani Afrika msimu ujao.

AS Vita Club yenye makao yake jijini Kinshasa, na TP Mazembe yenye makao yake mjini Lubumbashi zitacheza katika michuano ya klabu bingwa huku, Don Bosco ikicheza katika michuano ya Shirikisho.

Kinachosalia msimu huu ni kuwania taji la taifa “Congo Cup” .

Shirikisho la soka Fecofa limetangaza kuwa michuano ya kuwania hilo itaanza tarehe 10 hadi tarehe 23 mwezi Juni mjini Lubumbashi, jijini Kinshasa na mjini Bukavu.

Vlabu vinavyotaka kushiriki katika michuano hii vitahitajika kulipa Dola za Marekani 500 na vile vinavyotaka kushiriki vimepewa saa 72 kuwasilisha maombi yao kwa chama cha soka Fecofa.

Bingwa ni FC MK Etancheite.

Ex- CAF Media Expert. An expert on African football with over 15 years experience ,always with an ear to the ground with indepth knowledge of the game. I have worked for top publications including 7 years at www.supersport.com until i founded www.soka25east.com to quench the thirst of football lovers across the continent. I have trained young upcoming journalists who are now a voice in African football.I have covered World Cup,AFCON,CHAN,Champions League,Confederations Cup,Cecafa,Cosafa,Wafu and many other football tournaments across the World. Founder Football Africa Arena(FAA),Founder www.afrisportdigital.com

Bedjos Solutions Bondo

Must See

More in