Connect with us

CAF: Mataifa yatakayoshiriki fainali za Vijana yafahamika

CAF: Mataifa yatakayoshiriki fainali za Vijana yafahamika

Na Victor Abuso

Mataifa saba ya Afrika yatakayoshiriki katika michuano ya soka kuwania ubingwa wa Afrika kwa wachezaji wasiozidi miaka 23 itakayofanyika kati ya tarehe 28 mwezi Novemba hadi tarehe 12 mwezi Desemba nchini Senegal yameshafahamika rasmi
Mataifa hayo ni pamoja na wenyeji Senegal, Algeria, Misri, Zambia, Tunisia, Afrika Kusini, Nigeria na Mali.
Zambia, Tunisia na Mali zimefuzu katika michuano hii kwa mara ya kwanza.
Michuano ya mwisho ya kufuzu ilichezwa mwishoni mwa juma lililopita na washindi kupatikana.
Nigeria ilifuzu baada ya kuifunga Congo Brazaville mabao 2 kwa 1.
Algeria iliishinda Sierra Leone mabao 2 kwa 0, huku Mali ikiilaza Gabon mabao kwa 0.
Vijana wa Misri, waliwachabanga Uganda mabao 6 kwa 1, baada ya kushindwa mabao 4 kwa 0 jijini Cairo na nyumbani kulemewa kwa mabao 2 kwa 1.
Afrika Kusini nayo iliishinda Zimbabwe kwa jumla ya mabao 4 kwa 1, huku Tunisia wakiwalemea Morocco mabao 2 kwa 1.
Zambia baada ya kutoka sare ya kutofungana na Ivory Coast nyumbani na ugenini ilifuzu baada ya kupata ushindi wa penalti 4 kwa 3.
Michuano hiyo pia itatumiwa kutafuta timu tatu za kwanza kufuzu katika michezo ya msimu joto ya Olimpiki itakayofanyika nchini Brazil mwaka ujao.

Ex- CAF Media Expert. An expert on African football with over 15 years experience ,always with an ear to the ground with indepth knowledge of the game. I have worked for top publications including 7 years at www.supersport.com until i founded www.soka25east.com to quench the thirst of football lovers across the continent. I have trained young upcoming journalists who are now a voice in African football.I have covered World Cup,AFCON,CHAN,Champions League,Confederations Cup,Cecafa,Cosafa,Wafu and many other football tournaments across the World. Founder Football Africa Arena(FAA),Founder www.afrisportdigital.com

Bedjos Solutions Bondo

Must See

More in