Connect with us

CECAFA:Gor Mahia na Al Khartoum zafuzu nusu fainali

CECAFA:Gor Mahia na Al Khartoum zafuzu nusu fainali

Na Victor Abuso

Gor Mahia ya Kenya na Al Khartoum ya Sudan imefuzu katika hatua ya nusu fainali kuwania taji la klabu bingwa Afrika Mashariki na Kati CECAFA baada ya ushindi katika hatua ya robo fainali siku ya Jumanne katika uwanja wa taifa wa Dar es salaam nchini Tanzania.

Al Khartoum inayofunzwa na kocha wa zamani wa timu ya taifa ya Ghana Kwesi Apiah, ilipata ushindi mkubwa wa mabao 4 kwa 0 katika mchuano huo.

Bao la ufunguzi la Al Khartoum lilitiwa kimyani na mchezaji Atif Khalid katika dakika 10 ya mchuano huo, huku Amin Ibrahim akifunga bao la pili katika dakika ya 20 na 40 huku Osman Salaheldin akimaliza kazi kwa kuipa ushindi klabu yake bao la tano.

Kocha Appiah amesema kuwa mabao ya mapema yaliisaidia timu yake kuendelea kujiimarisha katika mchuano huo.

Katika mchuano mwingine, mabingwa wa Kenya Gor Mahia walipata ushindi wa mabao 2 kwa 1 dhidhi ya Malakia ya Sudan Kusini.

Gor Mahia ilipata bao lake la ufunguzi kupitia Godfrey Walusimbi katika dakika za mapema za mchuano huo ulionekana mgumu kwa vijana kutoka Kenya katika kipindi cha pili.

Mabingwa hao wa Kenya sasa watacheza na Al Khartoum katika hatua ya nusu fainali.

Siku ya Jumatano, Al Shandy washinda wa pili wa kundi B wanachuana na KCCA ya Uganda waliomaliza wa pili katika kundi C kwa alama 6.

Mchuano unaosubiriwa kwa hamu kubwa na mashabiki wa soka nchini Tanzania ni kati ya Azam na Yanga, mchuano ambao kwa mashabiki wa timu hizi mbili umekuja mapema na ni kama fainali ya mwaka 2013.

Fainali ya michuano hii ya CECAFA itachezwa siku ya Jumapili.

Ex- CAF Media Expert. An expert on African football with over 15 years experience ,always with an ear to the ground with indepth knowledge of the game. I have worked for top publications including 7 years at www.supersport.com until i founded www.soka25east.com to quench the thirst of football lovers across the continent. I have trained young upcoming journalists who are now a voice in African football.I have covered World Cup,AFCON,CHAN,Champions League,Confederations Cup,Cecafa,Cosafa,Wafu and many other football tournaments across the World. Founder Football Africa Arena(FAA),Founder www.afrisportdigital.com

Bedjos Solutions Bondo

Must See

More in