Connect with us

COSAFA:Namibia yafuzu robo fainali

COSAFA:Namibia yafuzu robo fainali

Na Victor Abuso,

Timu ya taifa ya soka ya Namibia imefuzu katika hatua ya robo fainali katika michuano ya kutafuta taji la COSAFA baina ya Mataifa ya Kusini mwa Afrika.

Namibia ilifuzu katika hatua hiyo kutoka kundi la A baada ya kumaliza kundi hilo kwa wingi wa alama saba na kupata ushindi muhimu Alhamisi usiku baada ya kuishinda Zimbabwe mabao 4 kwa 1.

Katika mchuano mwingine, Mauritius nao waliwashinda Ushelisheli bao 1 kwa 0.

Namibia sasa itamenyana na Zambia katika hatu hiyo ya robo fainali juma lijalo.

Leo ni michuano ya kumaliza kundi la B, na mchuano muhimu leo ni katia ya Madagascar na Swaziland kwa sababu ni timu moja tu ndio itakayofuzu katika hatua hiyo.

Madagascar na Swaziland zote zina alama 6.

Atakayefuzu atacheza na Ghana katika hatua ya nusu fainali.

Mchuano mwingine ni kati ya Tanzania na Lesotho zote ambazo zimeondolewa katika michuano hiyo kwa matokeo mabaya.

Tanzania ambayo imepata ukosoaji mkubwa kutoka kwa mashabiki wa soka nyumbani inalenga kupata ushindi leo usiku ili kurudi nyumbani na angalau kitu mkononi kutuliza hasira za mashabiki.

 

Sent from my Samsung device

Ex- CAF Media Expert. An expert on African football with over 15 years experience ,always with an ear to the ground with indepth knowledge of the game. I have worked for top publications including 7 years at www.supersport.com until i founded www.soka25east.com to quench the thirst of football lovers across the continent. I have trained young upcoming journalists who are now a voice in African football.I have covered World Cup,AFCON,CHAN,Champions League,Confederations Cup,Cecafa,Cosafa,Wafu and many other football tournaments across the World. Founder Football Africa Arena(FAA),Founder www.afrisportdigital.com

Bedjos Solutions Bondo

Must See

More in