Na Victor Abuso, Wapinzani Nigeria na Cameroon wametenganishwa katika michuano ya hatua ya makundi kuwania kombe la Afrika kwa vijana wasiozidi miaka 17 itakayochezwa mwaka 2019 nchini Tanzania. Droo hiyo ilifanyika Alhamisi usiku jijini Dar es salaam, kuelekea michuano hiyo itakayochezwa mwezi Aprili. Timu nyingine iliyopangwa katika kundi hilo ni pamoja na wenyeji Tanzania na jirani zao Uganda, ambao watacheza katika michuano hii kwa mara ya kwanza pamoja na Angola. Cameroon ambao walishinda taji hili mwaka 2003, wamepangwa katika kundi moja na Guinea, Morocco na Senegal. Michuano hiyo itatumiwa pia kutafuta nchi tatu, zitakazoliwakilisha bara la Afrika katika fainali za kombe la dunia nchini Peru mwaka ujao. Kundi A – Tanzania, Nigeria, Angola, Uganda Kundi B – Cameroon, Guinea, Morocco, Senegal. |
Droo ya vijana yataolewa Dar es salaam
Droo ya vijana yataolewa Dar es salaam
More in
-
CAF Announce dates CAF CL and CC Finals
The Confederation of African Football Caf has announced the dates of the two-legged Caf...
-
Yves Bissouma furious at being left out of Mali Squad
Tottenham midfielder Yves Bissouma is furious at being left out of the latest Mali...
-
Egypt beat New Zealand to qualify for Capital Cup final
Mostafa Mohamed scored the only goal of the game from the penalty spot in...
-
Nigeria Super Eagles beat Ghana Black Stars in Jollof Derby in Morocco
Nigeria Super Eagles bounced back from last month’s painful Africa Cup of Nations final...