Connect with us

Fainali ya Kombe la Shirikisho la Azam (ASFC) inatarajia kuchezwa Juni 2,2018 kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid,Arusha.

Katika mashindano ya ASFC mwaka huu kumefanyika maboresho ya kuongeza zawadi ambapo awali mshindi wa pili alikuwa hapati zawadi na katika msimu huu wa mashindano hayo mshindi wa pili atajikusanyia kiasi cha shilingi Milioni Kumi huku bingwa akibeba kitita cha shilingi Milioni Hamsini.

Zawadi nyingine zitakazotolewa ni pamoja na Mchezaji bora wa mashindano atakayezawadiwa shilingi milioni Moja,Kipa Bora atapata shilingi Milioni Moja huku mfungaji Bora pia akipata shilingi Milioni Moja wakati mchezaji Bora wa mchezo wa fainali akijizolea shilingi Laki Tano.

African journalist with passion of football reporting.Also i love politics

More in