Connect with us

Fainali ya vijana 2019: Misri kucheza mechi ya mwisho dhidi ya Mali

Fainali ya vijana 2019: Misri kucheza mechi ya mwisho dhidi ya Mali

Wenyeji Misri wanacheza mechi ya mwisho dhidi ya Cameroon, ikiwa ni hatua ya makundi, kuwania taji la vijana barani Afrika katika mchezo wa soka, kwa wachezaji waozidi miaka 23.

Mechi mbili zilizopita, Misri imeshinda michuano yote, na tayari imefuzu katika hatua ya mwondoano.

Mali ambao tayari wameondolewa katika michuano hii, baada ya kufungwa mechi mbili zilizopita, wanamaliza kazi na Ghana.

Michuani hii pia inatumiwa kufuzu kushiriki katika michuano ya Olimpiki mwaka ujao jijini Tokyo nchini Japan.

Katika michuano ya kundi B, mechi za kundi hilo yanamalizika siku ya Ijumaa. Nigeria, itachuana na Afrika Kusini, huku Ivory Coast ikimenyana na Zambia.

Afrika Kusini inaongoza kundi hilo kwa alama 4, huku Ivory Coast na Nigeria zikiwa na alama tatu.

Zambia ambayo pia inaweza kufuzu, ina alama moja.

Bedjos Solutions Bondo

Must See

More in