Connect with us

Kombe la dunia ni mashindano ya Kimataifa ya mchezo wa soka baina ya wanaume wanaowakilisha mataifa yao.

Michuano hii imekuwa ikichezwa tangu mwaka 1930 nchini Uruguay, chini ya usimamizi wa Shirikisho la soka duniani FIFA.

Fainali ya mwaka 2018 nchini Urusi, itakayofanyika kati ya tarehe 14 mwezi Juni hadi 15 mwezi Julai, itakuwa ya 21 katika historia ya michuano hiyo.

Michuano hii, hufanyika kila baada ya miaka minne.

Orodha ya Mataifa ambayo yamewahi kuwa wenyeji wa fainali ya kombe la dunia:-

1930-Uruguay

1934-Italia

1938-Ufaransa

1950-Brazil

1954-Switzerland

1958-Sweden

1962-Chile

1966-Uingereza

1970-Mexico

1974-West Germany

1978-Argentina

1982-Uhispania

1986-Mexico

1990-Italia

1994-Marekani

1998-Ufaransa

2002-Korea Kusini na Japan

2006-Ujerumai

2010-Afrika Kusini

2014-Brazil

2018-Urusi

Historia ya washindi wa kombe la dunia:-

Brazil-Mara 5 (1958,1962,1970, 1994 na 2002)

Ujerumani-Mara 4 (1954,1974,1990,2014)

Italia-Mara 4 (1934,1938,1982,2006)

Argentina-Mara 2 (1978,1986)

Uruguay-Mara 2 (1930,1950)

Ufaransa-Mara 1 (1998)

Uingereza-Mara 1 (1966)

Uhispania-Mara 1 (2010)

More in