Connect with us

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania(TFF) Ndugu Wallace Karia ameteuliwa kwa mara nyingine na Shirikisho la Mpira wa Miguu Barani Africa CAF kuwa kamishna wa mechi ya Morocco na Namibia kwenye fainali za Afrika kwa wachezaji wa ndani CHAN itakayochezwa Jumamosi Januari 27, 2018.

Mbali na Rais Karia Waamuzi watakaochezesha mchezo huo namba 22 utakaochezwa kwenye Uwanja wa Mohamed V Casablanca ni Mahamadou Keita  kutoka Mali  atakuwa mwamuzi wa katikati akisaidiwa na mwamuzi msaidizi namba moja kutoka Msumbiji Arsenio Chadreque Maringula na mwamuzi msaidizi namba mbili akitokea Burkina Faso  Seydou Tiama wakati mwamuzi wa akiba ni Ghead Grisha  akitokea Misri.

Hii ni mara ya tatu kwa Rais Karia kuteuliwa kuwa kamishna wa mechi zinazoendelea za fainali za Afrika kwa wachezaji wa ndani CHAN.

Aliteuliwa kuwa kamishna wa mechi ya ufunguzi ambapo Morocco walicheza na Mauritania Januari 13, 2018 na kisha akateuliwa tena kuwa kamishna wa mechi ya Namibia dhidi ya Zambia ambayo ilichezwa Januari 22, 2018

African journalist with passion of football reporting.Also i love politics

More in