Connect with us

Namibia wanyakua taji la COSAFA

Namibia wanyakua taji la COSAFA

Na Victor Abuso,

Timu ya taifa ya soka ya Namibia ndio mabingwa wa taji la COSAFA baina ya Mataifa ya Kusini mwa Afrika mwaka huu.

Brave Warriors, walinyakua taji hilo baada ya kuwashinda Msumbiji mabao 2 kwa 0 katika fainali iliyochezwa siku ya Jumamosi katika uwanja wa Moruleng nchini Afrika Kusini.

Mabao yote ya Namibia yalitiwa kimyani na Deon Hotto katika kipindi cha kwanza na cha pili cha mtanange huo.

Namibia imepata taji hili kwa mara ya kwanza tangu ilipofika katika hatua ya fainali mwaka 1997 na 1999 huku Msumbiji pia ikifika mwaka 2008.

Nafasi ya tatu ya michuano hiyo ilichukuliwa na Madagascar baada ya kuishinda Bostwana kwa mabao 2 kwa 1.

Mfungaji wa Madagascar alikuwa ni Sarivahy Vombola ambaye pia alimaliza michuano hiyo akiwa mfugaji bora akiwa na mabao matano.

Mechi 23 zilichezwa katika michuano hiyo huku mabao 46 yakifungwa.

Timu ya Tanzania na Ghana zilialikwa katika michuano hiyo.

Ex- CAF Media Expert. An expert on African football with over 15 years experience ,always with an ear to the ground with indepth knowledge of the game. I have worked for top publications including 7 years at www.supersport.com until i founded www.soka25east.com to quench the thirst of football lovers across the continent. I have trained young upcoming journalists who are now a voice in African football.I have covered World Cup,AFCON,CHAN,Champions League,Confederations Cup,Cecafa,Cosafa,Wafu and many other football tournaments across the World. Founder Football Africa Arena(FAA),Founder www.afrisportdigital.com

Bedjos Solutions Bondo

Must See

More in