Connect with us

Timu ya Taifa ya Vijana chini ya miaka 20 (Ngorongoro Heroes) itacheza na timu ya Taifa ya Mali U20 Jumapili Mei 13,2018 Uwanja wa Taifa Dar es Salaam.

Katika mchezo huo utakaochezwa saa 10 jioni kiingilio cha kuingia Uwanjani kutazama mechi hiyo VIP zote shilingi 3,000 Mzunguko shilingi 1,000.

Ngorongoro Heroes wapo kambini wakiendelea kujiandaa na mchezo huo,leo wapo kwenye ratiba ya kufanya mazoezi ya gym asubuhi na jioni kabla ya kuwa na mazoezi ya uwanjani kesho na Ijumaa ambapo kesho Alhamisi watakuwa na kipindi kimoja cha Uwanjani saa 10 kwenye Uwanja wa Uhuru wakati Ijumaa watafanya vipindi viwili asubuhi na jioni saa 10.

Kikosi hicho hakina majeruhi vijana wana morali kubwa ya kufanya vizuri katika mchezo huo wa kwanza wa raundi ya pili ya kufuzu fainali za vijana Africa.

African journalist with passion of football reporting.Also i love politics

More in