Connect with us

Serikali ya Tanzania imeunda kamati inayohusihs viongozi mbalimbali wa soka kwa ajili ya maandalizi ya fainali za Afrika za vijana chini ya miaka 17 zitakazofanyika nchini humo mwa 2019.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo wa Serikali ya Tanzania Dr. Harrison Mwakyembe ametangaza majina ya wajumbe wa kamti hiyo ambao jukumu lao kubwa litakuwa ni kuhakikisha Tanzania inaandaa kikamilifu fainali hizo.

Waziri Mwakyembe amesema Tanzania ina kazi kubwa kuhakikisha inaandaa fainali hizo.

“Kama unavyofahamu, Tanzania ilipokea heshima ya kuandaa mashindano ya AFCON 2019 kwa vijana chini ya miaka 17 baada ya mashindano kama hayo kufanyika Libreville, Gabon mwezi Mei, mwaka huu.

“Ili kufanikisha maandalizi ya mashindano hayo ya Afrika nimezindua Kamati ya Maandalizi inayojumuisha viongozi wa Serikali na wadau mbalimbali wa Michezo kwa kuzingatia kanuni za Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani (FIFA) na Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF).

Kabla ya kuzindua kamati hiyo, Mhe. Waziri Mwakyembe alisema: “2019 tuna mtihani. Mtihani mkubwa. Na lazima tuufaulu. Tuna ugeni mkubwa ambao kamati itakuwa na kazi ya kufanya maandalizi haya kwa kazi ya kujitolea. Walioteuliwa ni watu wote wana rekodi na uzoefu mzuri kwenye masuala ya michezo.”

Uzinduzi wa kamati hiyo ulifanyika Ukumbi wa Watu Maalumu (VIP) katika Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam ambako Mhe. Waziri Dk. Mwakyembe alikubali kuwa Mwenyekiti wa Kamati huku Makamu Mwenyekiti wake akiwa ni Rais wa Heshima wa TFF, Leodegar Chilla Tenga ilihali Mtendaji Mkuu atakuwa Dk. Henry Tandau.

Wajumbe ni Makamu Rais wa TFF, Michael Wambura na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda; Dk. Damas Ndumbaro ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Rufaa za Leseni za Klabu ya TFF; Dk. Francis Michael wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam – Kitivo cha Sheria; Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Mohammed Enterprises, Mohammed Dewji na Mkurugenzi Mtendaji wa Makampuni ya Said Salim Bakhressa, Abubakar Bakhressa.

Pia wamo Yussuph Singo Omari – Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo katika Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo; Ahmed Msafiri Mgoyi – Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano ya TFF; Khalid Abdallah – Mwenyekiti Kamati ya Maendeleo ya Vijana ya TFF kadhalika Dk. Hamis Kigwangalla – Waziri wa Maliasili na Utalii.

Wajumbe wengine ni Nassib Mmbagga – Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Temeke; Dar es Salaam; Angetile Osiah Mhariri Mwandamizi wa Magazeti ya Kampuni ya Mwananchi Communications; Dk. Allain Kijazi – Mkurugenzi Mkuu TANAPA; Dk. Dotto James – Katibu Mkuu, Wizara ya Fedha na Mipango; Dk. A. P. Makakala – Kamishna Jenerali Idara ya Uhamiaji; Dk. Fredy Manongi – Mkurugenzi Mkuu Hifadhi ya Ngorongoro.

Wamo pia Lameck Nyambaya – Mjumbe Kamati ya Utendaji ya TFF; Mkurugenzi Mkuu wa PPF, William Erio; Kelvin Twissa – Ofisa Masoko Mkuu Sportpesa; Profesa Lawrence Museru – Mkurugenzi Mkuu Hospitali ya Taifa ya Muhimbili; Injinia Ladislaus Matindi – Mkurugenzi Mtendaji ATCL na Devotha Mdachi – Mkurugenzi Bodi ya Utalii Tanzania.

Pamoja na Wajumbe hao, wengine wanaoingia kwenye kwa nafasi zao katika Kamati hiyo ya maandalizi ni Rais wa TFF na Katibu Mkuu wa TFF.

African journalist with passion of football reporting.Also i love politics

More in