Connect with us

Tanzania:Yanga FC kupata Shilingi Milioni 80 za Kitanzania kwa kushinda ligi

Tanzania:Yanga FC kupata Shilingi Milioni 80 za Kitanzania kwa kushinda ligi

Na Victor Abuso,

Yanga FC, mabingwa wa ligi kuu ya soka Tanzania bara msimu huu, watakabidhiwa kitita cha Shilingi za Kitanzania Milioni 80 na Laki Nne baada ya kushinda taji hilo.

Wafadhili wakuu wa ligi hiyo kampuni ya simu ya mkononi Vodacom, wamethibtisha hilo na kuongeza kuwa Azam FC waliomaliza katika nafasi ya pili watapata kitita cha Shilingi Milioni 40, huku Simba FC iliyomaliza ya tatu ikikabidhiwa Shilingi Milioni 28.

Mkuu wa kitego cha Uhusiano mwema katika kampuni hiyo Matina Nkurlu amedokeza mwishoni mwa juma kuwa mfungaji bora msimu huu Simon Msuva kutoka Yanga FC naye atapata Shilingi Milioni 5.

Kipa bora naye atapata Milioni 5 sawa na mchezaji bora wa mwaka huku kocha bora na mwamuzi bora pia watatuzwa.

Wafadhili wa ligi Tanzania bara wanasema wanatoa zawadi hizi ili kuinua kiwango cha soka na kuhimiza ushindani na kutafuta vipaji miongoni mwa vijana nchini humo.

Sherehe ya kuwatuza washindi wa ligi msimu huu zitafanyika katikati ya mwezi wa Juni jijini Dar es salaam.

Ex- CAF Media Expert. An expert on African football with over 15 years experience ,always with an ear to the ground with indepth knowledge of the game. I have worked for top publications including 7 years at www.supersport.com until i founded www.soka25east.com to quench the thirst of football lovers across the continent. I have trained young upcoming journalists who are now a voice in African football.I have covered World Cup,AFCON,CHAN,Champions League,Confederations Cup,Cecafa,Cosafa,Wafu and many other football tournaments across the World. Founder Football Africa Arena(FAA),Founder www.afrisportdigital.com

Bedjos Solutions Bondo

Must See

More in