Connect with us

TP Mazembe kujipima nguvu na Azam FC

TP Mazembe kujipima nguvu na Azam FC

Na Victor Abuso,

Mabingwa mara nne wa taji la klabu bingwa barani Afrika TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo watamenyana na mabingwa wa CECAFA, Azam FC ya Tanzania katika mchuano wa kirafiki wa Kimataifa.

Mchuano huo utaisaidia Mazembe katika mechi yake ya kuwania taji la klabu bingwa barani Afrika CAF dhidi ya Al Hilal ya Sudan tarehe 23 mwezi huu.

Afisa Mkuu wa klabu ya Azam, Saad Kawemba ameliambia Gazeti la The Citizen kuwa mchuano huo pia utawasaidia kwa maandalizi ya ligi kuu ya Tanzania bara mwezi ujao lakini pia mchuano wa hisani ya ngao dhidi ya Yanga tarehe 22 mwezi huu.

Mbali na TP Mazembe, Matajiri hao wa jiji la Dar es salaam wamepiga kambi visiwani Zanzibar kwa maandalizi yake lakini pia imeratibiwa kumenyana na Zesco United ya Zambia na Silver Strikes ya Malawi katika michuano mingine ya kirafiki.

Mwishoni mwa juma lililopita, Mazembe ikiwa nyumbani katika uwanja wake mjini Lubumbashi iliifunga Smouha ya Misri bao 1 kwa 0 na sasa inaongoza kundi lao kwa alama nane.

Huu ni ushindi wa pili dhidi ya klabu hii ya Misri kwa sababu mchuano wa kwanza mjini Alexandria mwezi uliopita, TP Mazembe walipata ushindi wa mabao 2 kwa 0 wakiwa ugenini.

 

Ex- CAF Media Expert. An expert on African football with over 15 years experience ,always with an ear to the ground with indepth knowledge of the game. I have worked for top publications including 7 years at www.supersport.com until i founded www.soka25east.com to quench the thirst of football lovers across the continent. I have trained young upcoming journalists who are now a voice in African football.I have covered World Cup,AFCON,CHAN,Champions League,Confederations Cup,Cecafa,Cosafa,Wafu and many other football tournaments across the World. Founder Football Africa Arena(FAA),Founder www.afrisportdigital.com

Bedjos Solutions Bondo

Must See

More in