Connect with us

Uganda:Lweza FC washushwa daraja kwa kukosa uwanja

Uganda:Lweza FC washushwa daraja kwa kukosa uwanja

Na Victor Abuso,

 

Klabu ya soka ya Lweza FC nchini Uganda, ina siku mbili kukata rufaa dhidi ya hatua ya Shirikisho la soka nchini humo kuwashusha daraja.

Kamati ya FUFA, inasema kuwa klabu hiyo kutoka mitaa ya Kajjansi imeshindwa kutimiza masharti ya kuendelea kushiriki katika ligi kuu msimu huu licha ya kusalia katika ligi hiyo msimu uliopita.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo Bernard Ogwel amesema uongozi wa Lweza FC umeshindwa kuthibitisha umiliki wa uwanja wao, mikataba ya wachezaji, viongozi wa klabu hiyo na kocha wake.

Ogwel amesisitiza kuwa kwa sababu klabu hiyo iliyoshiriki ligi kuu msimu uliopita, haijatekelaza masharti hayo, imeshushwa daraja.

Hata hivyo, msemaji wa klabu hiyo Abdul Suleiman Semugenyi amesema klabu yake itatekeleza masharti hayo yote kabla siku ya Ijumaa wiki hii.

Masaibu ya klabu hii iliyozinduliwa mwaka 1990 katika mtaa wa Kajjansi jijini Kampala, yanakuja baada ya kutangazwa mabingwa wa taji la Vipers mwaka 2015.

 

 

Ex- CAF Media Expert. An expert on African football with over 15 years experience ,always with an ear to the ground with indepth knowledge of the game. I have worked for top publications including 7 years at www.supersport.com until i founded www.soka25east.com to quench the thirst of football lovers across the continent. I have trained young upcoming journalists who are now a voice in African football.I have covered World Cup,AFCON,CHAN,Champions League,Confederations Cup,Cecafa,Cosafa,Wafu and many other football tournaments across the World. Founder Football Africa Arena(FAA),Founder www.afrisportdigital.com

Bedjos Solutions Bondo

Must See

More in