Connect with us

Vigogo wa soka nchini Uganda wapata kazi CAF

Vigogo wa soka nchini Uganda wapata kazi CAF

Na Victor Abuso,

Rais wa Shirikisho la soka nchini Uganda FUFA, Moses Magogo na Mkurugenzi Mkuu Mtendaji wa Shirikisho hilo Edgar Watson wameteuliwa kuhudumu katika kamati za Shirikisho la soka barani Afrika CAF.

Hii inafika idadi ya raia wa Uganda wanaoketi katika kamati za CAF kufikia watano.

Rais wa FUFA, ametajwa kuwa mwanachama wa Kamati ya kupanga michuano ya klabu bingwa barani Afrika, huku Edgar Watson akishiriki katika Kamati ya kiufundi na maendeleo.

Mkuu wa maswala ya Sheria wa Fufa, Alex Luganda ameendelea kushikilia nafasi ya ukataji rufaa, huku James Sekajugo akiendelea kuketi katika Kamati ya afya.

Rais wa zamani wa FUFA, Lawrence Mulindwa naye ni mwanachama katika kamati inayoandaa michuano ya vijana walio na umri wa chini ya miaka 20 barani Afrika.

Wanakamati hao wapya wa CAF watahudmu kwa muhula wa miaka miwili.

Ex- CAF Media Expert. An expert on African football with over 15 years experience ,always with an ear to the ground with indepth knowledge of the game. I have worked for top publications including 7 years at www.supersport.com until i founded www.soka25east.com to quench the thirst of football lovers across the continent. I have trained young upcoming journalists who are now a voice in African football.I have covered World Cup,AFCON,CHAN,Champions League,Confederations Cup,Cecafa,Cosafa,Wafu and many other football tournaments across the World. Founder Football Africa Arena(FAA),Founder www.afrisportdigital.com

Bedjos Solutions Bondo

Must See

More in