Connect with us

 

Al-Merrikh ya Sudan, KCCA ya Uganda, AS Vita Club ya DRC na Yanga ya Tanzania zimefuzu katika mzunguko wa kwanza kuwania taji la klabu bingwa barani Afrika mwaka 2017.

Vlabu hivi vilifuzu baada ya kumalizika kwa michuano ya marudiano hatua ya wali mwishoni mwa wiki iliyopita, zilizopigwa katika viwanja mbalimbali barani Afrika.

Michuano ya mzunguko wa kwanza, itachezwa mwezi Machi nyumbani na ugenini na mshindi atafuzu katika hatua ya makundi.

KCCA itamenyana na Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini ambao ndio mabingwa watetezi wa taji hili, huku Rivers United ya Nigeria ikimenyana na Al-Merrikh ya Sudan.

Yanga ya Tanzania itamenyana na Zanaco ya Zambia. Zanaco ilifuzu baada ya kuishinda APR ya Rwanda katika hatua ya awali.

AS Vita Club nayo itatafuta nafasi ya kufuzu na itamenyana na Gambia Ports Authority huku TP Mazembe ya DRC ikimenyana na CAPS United ya Zimbabwe.

Ratiba nyingine ya michuano ya klabu bingwa:-

Al-Hilal vs AS Port-Louis 2000

AC Leopards vs Saint George

Al-Ahly vs Bidvest Wits

Coton Sport vs CnaPS Sport

Zamalek vs Enugu Rangers

Ferroviario Beira vs Stade Malien

Wydad Casablanca vs CF Mounana

Al-Ahli Tripoli vs FUS Rabat

Esperance de Tunis vs Horoya

Etoile du Sahel vs AS Tanda

USM Alger vs Rail Club du Kadiogo

Vlabu 16 vitafuzu katika hatua ya makundi na kugawanywa katika makundi manne, kila kundi na vlabu vinne.

More in