Connect with us

Wachezaji wa AFC Leopards waenguliwa katika kikosi cha Harambee Stars

Wachezaji wa AFC Leopards waenguliwa katika kikosi cha Harambee Stars

Na Victor Abuso,

Kocha wa timu ya taifa ya soka ya Kenya Harambee Stars Bobby Williamson amewaacha wachezaji wa klabu ya AFC Leopards baada ya uongozi wa klabu hiyo kuamuru kuwa warudi kambini kuendelea na maandalizi ya kuwania taji la ligi kuu.

Harambee Stars imekuwa ikijiandaa katika michuano ya kufuzu kombe la mataifa bingwa barani Afrika mwaka 2017 nchini Gabon na hatua hii ya uongozi wa AFC inaamanisha kuwa wachezaji hao watakosa kuliwakilisha taifa.

Kenya itaanza safari ya kusaka tiketi hiyo dhidi ya Congo Brazaville Jumamosi ijayo ugenini.

Kikosi cha Williamson kinaelekea jijini Kigali nchini Rwanda siku ya Ijumaa kuanza kambi na pia kushiriki katika mchuano wa kimataifa wa kirafiki dhidi ya Tanzania siku ya Jumamosi.

Wachezaji wa Gor Mahia wataungana na wachezaji wengine baada ya mchuano wao wa ligi kuu dhidi ya Tusker mjini Kisumu.

Nahodha wa Stars ni Victor Wanyama anayecheza soka la kulipwa katika klabu ya Southamptom nchini Uingereza , anaongoza kikosi cha wachezaji wakulipwa kuiwakilisha Kenya katika mchuano huo wa kimataifa.

Mbali na Congo Brazavile, Kenya imejumuishwa pamoja na Zambia na Guine Bissau.

Kikosi kamili

Makipa:

Goalkeepers: Joseph Baraza and Ian Otieno(Rangers)

Mabeki: Charles Odette(Sony Sugar) , Evans Maliachi(Muhoroni Sugar), David Ochieng(Al Tawoon), Brian Mandela(Santos)

Viungo wa Kati: Antony Akumu(Al Khartoum), Stephen Wakanya(Chemelil), Peter Nzuki(Nakumatt), Victor Wanyama(Southampton)

Washambulizi: Allan Wanga(Al M ereikh), Francis Kahata(FK Tirana).

Wachezaji wa Gor Mahia watakaojiunga na wenzao jijini Kigali ni pamoja na, Musa Mohammed, Harun Shakava,Victor Ali Abondo,Bonface Oluoch,Collins Okoth,Michael Olunga na kipan wa makipa Mathew Ottamax.

Ex- CAF Media Expert. An expert on African football with over 15 years experience ,always with an ear to the ground with indepth knowledge of the game. I have worked for top publications including 7 years at www.supersport.com until i founded www.soka25east.com to quench the thirst of football lovers across the continent. I have trained young upcoming journalists who are now a voice in African football.I have covered World Cup,AFCON,CHAN,Champions League,Confederations Cup,Cecafa,Cosafa,Wafu and many other football tournaments across the World. Founder Football Africa Arena(FAA),Founder www.afrisportdigital.com

Bedjos Solutions Bondo

Must See

More in