Connect with us

Yanga yajiweka pazuri kutetea taji la ligi kuu

Yanga yajiweka pazuri kutetea taji la ligi kuu

 

Klabu ya soka ya Yanga imeendelea kuongoza ligi kuu nchini humo na kuweka nia ya dhati ya kutetea taji lake baada ya mwishoni mwa Juma lililopita baada ya kuwashinda Toto Africans mabao 2 kwa 1 katika uwanja wa CCM Kirumba huko Mwanza.

Matokeo hayo yaliwapa wanajangwani alama tatu muhimu na kuiweka kileleni kwa alama 62.

Simba na Azam FC nao walikuwa na kibarua kujaribu kuwafikia Yanga lakini timu hizi mbili zilitoka sare ya kutofungana katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.

Azam inasalia katika nafasi ya pili kwa alama 59 na Simba ikiwa na alama 58.

Ratiba Jumatano Mei 4 2016

  • Azam FC vs JKT Ruvu

Mei 7 2016 Jumamosi

  • JKT Ruvu vs Ndanda FC
  • Kagera Sugar vs Azam FC
  • Simba SC vs Mwadui FC.
Bedjos Solutions Bondo

Must See

More in