Connect with us

Cameroon yaanza vema michuano ya vijana

Cameroon, mabingwa wa mwaka 2003 katika taji la soka barani Afrika kwa vijana wasiozidi miaka 17, wameanza vema mashindano yanayoendelea nchini Tanzania.

Lions Indomptables waliifunga Guinea mabao 2-0 katika mechi iliyochezwa katika uwanja wa Chamazi, nje kidogo ya jiji la Dar es salaam.

Morocco na Senegal nazo zilitoka sare ya bao 1-1 katika mechi ya pili ya kundi B.

Cameroon inaongoza kundi la B kwa alama tatu huku Morocco, Senegal na Guinea zikiwa na alama moja.

Michuano hii itarejelewa siku ya Jumatano.

Nigeria inayoongoza kundi la A kwa alama tatu, itamenyana na Uganda baada ya kuwashinda wenyeji Tanzania mabao 5-4.

Tanzania nayo itachuana na Angola, ambayo mechi ya kwanza iliishinda Uganda bao 1-0.

Bedjos Solutions Bondo

Must See

More in