Connect with us

Kahata yuko salama,Mkude,Chama,Erasto kuhojiwa na kamati ya nidhamu Simba

Kahata yuko salama,Mkude,Chama,Erasto kuhojiwa na kamati ya nidhamu Simba

Na mwandishi wetu Akira Dar Es Salaam,

Baada ya kuzuka na kusambaa kwa taarifa katika mitandao mbalimbali ya kijamii na baadhi ya vyo vya habari kuhusiana na wachezaji wa Simba SC kudaiwa kugoma.

Afisa mtendaji mkuu wa Simba SC Senzo Masingiza ametoa taarifa rasmi kuhusiana na msimamo wa klabu hiyo, awali iliripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari kuwa wachezaji wa Simba SC Erasto Nyoni, Francis Kahata, Clotous Chama, Jonas Mkude na Gadiel Michael wamegomea baadhi ya michezo ya Simba ili kushinikiza walipwe pesa zao za usajili.

Wachezaji hao walikosekana katika michezo ya Kagera Sugar Septemba 26 mjini Bukoba na Biashara United Septemba 29 mjini Musoma, taarifa iliyotolewa na Simba SC inaeleza kuwa wachezaji hao wakirejea timu zao za taifa watahojiwa na kamati ya nidhamu ila Francis Kahata alikuwa na ruhusa maalum ya kwenda Kenya kushughulikia.

Bedjos Solutions Bondo

Must See

More in