Connect with us

Michuano ya Mapinduzi yaendelea kurindima Zanzibar

Michuano ya Mapinduzi yaendelea kurindima Zanzibar

Michuano ya kuwani taji la Mapinduzi Visiwani Zanzibar, inaedelea leo Jumanne katika uwanja wa Amman.

Mafunzo ya Zanzibar watachuana na Mtibwa Sugar kutoka Tanzania bara kuanzia saa 10 na nusu jioni.

Azam FC nayo itapambana na Yanga kuanzia saa mbili na dakika 15 usiku.

Michuano ya leo ni ya kundi B.

IMG_6010-1024x683

Jana, Jumatatu, URA iliishinda JKU ya Zanzibar mabao 3 kwa 1.

Simba nayo ilitoka sare ya mabao 2 kwa 2 na Jamhuri FC.

Oscar Agaba alikuwa wa kwanza kuifungia URA bao la kwanza katika dakika ya 12 ya mchuano huo lakini Nasser Juma akaisawazishia JKU dakika tano baadaye lakini URA ilipata bao la ushindi katika dakika ya 22 kipindi cha kwanza.

URA watarejea uwanjani siku ya Jumatano kumenyana na mabingwa watetezi Simba.

Nusu fainali itachezwa siku ya Jumamosi na Jumapili huku fainali ikiratibiwa kuchezwa siku ya Jumatano juma lijalo.

Bedjos Solutions Bondo

Must See

More in