Connect with us

Nigeria: Sunday Oliseh ajiuzulu

Nigeria: Sunday Oliseh ajiuzulu

 

Sunday Oliseh amejiuzulu kuwa kocha wa timu ya taifa ya soka ya Nigeria, Super Eagles.

Hatua hii inakuja miezi saba baada ya kupewa kibarua hicho na Shirikisho la soka nchini humo NFF.

Mchezaji huyo wa zamani wa Super Eagles alitangaza kujiuzulu kwake, kupitia ukurasa wake wa Twitter kwa kile alichokisema NFF imevunja masharti ya mkataba wake.

Aidha, anadai kuwa Shirikisho la soka nchini humo limeshindwa kumuunga mkono katika kazi yake, kutomlipa marupurupu yake pamoja na wachezaji wake.

Kwa sababu ya kutoheshimiwa kwa mkataba wangu, kutoungwa mkono, kutolipwa marupurupu yangu pamoja na yale ya wachezaji wangu, najiuzulu kama kocha wa Super Eagles,” aliandika Oliseh kupitia ukurasa wake wa Twitter.

Pamoja na hayo, Oliseh amewashukuru raia wa Nigeria kwa kumuunga mkono wakati alipokuwa kocha wa timu ya taifa.

Mwaka uliopita, Oliseh alitofautiana na kipa Vincent Enyeama, na baadaye akaamua kustaafu kuichezea timu ya taifa.

Shirikisho la soka nchini Nigeria linasema bado halijapokea rasmi barua ya Oliseh kuonesha kujiuzulu kwake.

 

Bedjos Solutions Bondo

Must See

More in