Connect with us

Uchambuzi: Nick Mwendwa atumbue majipu Kenya

Uchambuzi: Nick Mwendwa atumbue majipu Kenya

Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli anafahamika kwa usemo wa hapa kazi tu, na wengine wanamwita Mzee wa kutumbua majipu kutokana na jitihada zake za kupambana na ufisadi na kuhakikisha kuwa taifa hilo linakuwa na watu wanaofanya kazi kwa bidii.

Huu ni usemi mwafaka, kwa rais mpya wa Shirikisho la soka nchini Kenya Nick Mwendwa aliyechaguliwa siku ya Jumatano jijini Nairobi.

Kumekuwa na madai ya kufujwa kwa fedha kutoka FIFA za kuendeleza soka na pia zile kutoka serikalini, wachezaji wa timu ya taifa kutolipwa kwa wakati lakini pia kufutwa kazi kwa makocha wa timu ya taifa.

Mwendwa kwa kupata kura 50 katika uchaguzi huo na kumshinda Mwenyekiti wa klabu ya Gor Mahia Ambarose Rachier, inaonesha imani na kiu waliyonao Wakenya kutaka mabadiliko katika mchezo wa soka.

Kenya imekuwa ikishindwa kuendeleza soka la vijana na kuisababishia Harambee Stars katika mechi mbalimbali za Kimataifa.

Rais huyo mypa mwenye umri wa miaka 37, aliongoza vuguvugu lililotaka mabadiliko “Team Change” na ndio kitu ambacho wapenzi wa soka nchini Kenya wanataka kukiona.

Kazi ni kwa Nick Mwendwa ambaye sasa anahitaji ushirikiano wa wadau wote wa soka.

Huu ni mwamko mpya wa soka soka nchini Kenya.

Viongozi waliowahi kuongoza soka nchini Kenya:-

1963-1964 Isaac Lugonzo

1964-1968  John Kasyoka

1968–1970Kamati maalum ikiongozwa Jonathan Njenga

1970-1973   Martin Shikuku

1973 Kamati maalum ikiongozwa Billy Martin

1973-1974    William Humphrey Ngaah

1974-1975 Dan Owino

1975-1978   Kenneth Matiba

1978-1980 Dan Owino

1980–1984 Clement Gachanja

1984-1992 Job Omino

1992-1996 Kamati maalum ikiongozwa Matthew Adams Karauri

1996-2000   Peter Kenneth

2001-2004 Maina Kariuki

2004 Kamati maalum ikiongozwa Kipchoge Keino

2004-2007  Alfred Sambu

2007–2011   Mohamed Hatimy

2011–2015 Sam Nyamweya

2016- Nick Mwendwa

Bedjos Solutions Bondo

Must See

More in